Deuteronomy 9:20-22

20Bali yeye alimkasirikia Haruni kiasi cha kutaka kumwangamiza, nami wakati huo nilimwombea Haruni pia. 21 aKisha nikachukua ile sanamu ya ndama mliyoitengeneza na kuichoma kwenye moto. Nikaiponda na kuisaga ikawa unga laini kama vumbi, nikatupa lile vumbi kwenye kijito kilichotiririka toka mlimani.

22 bPia mlimkasirisha Bwana huko Tabera, Masa na Kibroth-Hataava.

Copyright information for SwhKC